ATUHUMIWA KUIBA MTOTO

 


MAMA wa mtoto aliyeibwa kabla hajatimiza mwezi tangu azaliwe, Fatuma Bakari ameieleza Mahakama ya Wilaya ya Ilala jinsi mtoto huyo alivyoibwa na mshtakiwa Neema Patrick. 

Shahidi huyo na mwingine walitoa ushahidi wao jana mbele ya Hakimu Adelf Shachore kwa kuongozwa na Wakili wa Serikali, Anunciata Leopold. 

Awali mashahidi hao walikuwa watano ambao walifika mahakani kwa ajili ya kutoa ushahidi, lakini Wakili Leopold, alidai kuwa kwa mujibu wa shtaka hilo waliotakiwa kutoa ushahidi walikuwa wawili tu. 

Wakitoa ushahidi wao mashahidi hao ambao ni Fatuma Bakari na Zainabu Said, wote walikiri juu ya mtuhumiwa kufanya kitendo hicho cha kuiba mtoto. 

“Ni kweli siku ya tukio ambayo ni mwezi machi mwaka huu, mtuhumiwa alinisindikiza hospital nilipokuwa naumwa jino, kutokana na hali niliyokuwa nayo mtuhumiwa aliniomba anibebee mwanangu (Ibrahm Abdalah, ambaye hajatimiza hata mwezi) lakini mara baada ya kufika hospital maeneo ya Mbagala, Dar es Salaam, alishushuka haraka na kukimbia na mwanangu,” alidai Shahidi huyo. 

Awali mashahidi hao walitakiwa kuwa watano lakini wakili wa serikali alipinga kutoa utetezi wao, hivyo mashahidi watatu walibaki ushahidi wao utasikilizwa Juni 24 mwaka huu. 

Mtuhumiwa huyo anadaiwa kumwiba mtoto huyo maeneo ya Mbagala Machi 3 mwaka huu ambapo alikuja kukamatwa baad ya wiki mbili maeneo ya Ukonga Banana akiwa na mtoto huyo, mtuhumiwa huyo yuko nje kwa dhamana.

Kortini kwa Kumpa Mwanafunzi Mimba





MKAZI wa Mpiji Magoe Hamis Mohameid (21), amefikishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni Dar es Salaam akikabiliwa na tuhuma za kumbaka mwanafunzi (14)Jina limehifadhiwa na kumpa mimba. 

Akisomewa mashtaka mawili mbele ya Hakimu Flora Mtarania, Wakili wa Serikali Grace Lwila, alidai kuwa tukio hilo lilitokea kati ya Aprili na Mei24 mwaka huu maeneo ya huko Mpiji Magoe. 

Katika shtaka la kwanza Wakili alidai kwamba mtuhumiwa alimbaka msichana huyo kisha kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri. 

Wakili Lwila alidai kuwa katika shtaka la pili katika tarehe isiyojulikana maeneo ya Mpiji Magoe mtuhumiwa alimpa ujauzito mwanafunzi huyo wa kidato cha pili anayesoma shule ya Sekondari Mpiji Magoe. 

Mtuhumiwa alikana kutenda shtaka hilo na upelelezi wa shauri hilo bado unaendelea ambapo Hakimu Mtarania alisema kwamba shauri hilo linadhaminika. 

“Unatakiwa ulete wadhamini wawili walioajiriwa kutoka serikalini au katika taasisi inayotambulika kisheria watakaoweka bondi ya maandishi ya Sh. Milioni 1,” alisema Mtarania. 

Hata hivyo mtuhumiwa alirudishwa mahabusu kwa kushindwa kutimiza masharti hayo na kesi hiyo itakuja tena Juni 24, mwaka huu.

Sita wafa katika ajali, 45 wajeruhiwa Singida

 

WATU sita wamekufa na wengine 45 kujeruhiwa katika ajali mbili tofauti za barabarani zilizotokea juzi na jana mkoani Singida. 

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Thobias Sedoyeka alisema mjini hapa jana kuwa ajali ya kwanza ilitokea Juni 11 mwaka huu saa 1.30 usiku eneo la Manga nje kidogo ya mji huu kwenye Barabara Kuu ya Singida – Mwanza. 

Alisema ajali hiyo ililihusisha basi lenye usajili wa namba T174 CAV Scania la Kampuni ya Nice Line linalomilikiwa na Enock Mwita wa jijini Mwanza ambalo lilikuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Mwanza. 

Dereva wa basi hilo aliligonga kwa nyuma gari la mizigo lenye namba za usajili RAT 317N/ RL 0754 aina ya Benz lililokuwa limeegeshwa pembeni mwa barabara hiyo na kusababisha vifo vya abiria watatu papo hapo. Wengine wawili walifia hospitalini na kusababisha majeruhi 37. 

Kwa mujibu wa Kamanda Sedoyeka, dereva huyo ambaye alikimbilia kusikojulikana baada ya ajali kutokea, alikuwa kwenye mwendo kasi. Katika ajali nyingine iliyotokea Juni 12 saa 12.15 asubuhi katika eneo la Kindai kwenye barabara kuu ya Singida – Dodoma nje kidogo ya mji huu, gari aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T 998 CWG liliacha njia na kupinduka kisha kusababisha kifo cha abiria mmoja na majeruhi wanane. 

Alisema abiria wa gari hilo walikuwa wakisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Kahama mkoani Shinyanga kwa ajili ya kuhudhuria mazikoi ya ndugu yao na gari lao lilipofika eneo la ajali kwenye kona kali dereva wake, Paul Bundala alishindwa kulimudu kutokana mwendo kasi. 

Baadhi ya waliokufa katika ajali hiyo ni Shija Masanja,Yohana Chimole na Febronia Kway. Miili ya waliotajwa na wengine watatu ambao majina yao hayajatambuliwa imehifadhiwa katika hospitali ya mkoa wa Singida ambapo pia wamelazwa majeruhi.
-chanzo:mpekuzi

Naombeni ushauri...Mjomba kaingia chumbani Kwangu Akanikuta Navaa Nguo sasa Anataka. Nifanyaje, ameniambia nikikataa atanifukuza?

 
Baba mdogo wangu ananitaka kimapenzi, alikuja gafla chumbani kwangu na kuingia bila kupiga hodi kuniambia kwamba mama amezimia gafla kutokana na ugonja wa kifafa unaomsumbua.


Bahati mbaya wakati anaingia chumbani kwangu gafla alinikuta nikiwa uchu nikiwa nimevaa chupi tu, sasa toka wakati huo amakua akiniangalia kwa macho ya kimapenzi na anataka kutoka na mimi out anasema kuna jambo anataka kuongea na mimi.

Nimefikiria kumwambia kaka yake , lakini nahisi nikimwambia baba naweza kufanya tatizo kuwa kubwa zaidi, naombeni ushauri wanajamii forums, sababu sasa ameanza kunitumia message za mapenzi usiku, na huyu ni baba yangu mdogo na amenipita miaka mingi kwa kweli, namheshimu na naogopa kumjibu vibaya.

18+ KANGA MOKO NDEMBE NDEMBE....HAYA NDIO YANAYOFANYIKA JUKWAANI KATIKA SHOW ZA USIKU




Lulu Atoboa Sababu ya Kutofanya ‘Movie’kwa Mwaka Mzima


Staa wa Bongo Movies, Elizabeth Michael,’Lulu’amefunguka sababu ya kutofanya filamu kwa mwaka mzima kuwa alikuwa bize na shughuli zingine ikiwemo masomo.

Akizungumza na Clouds Fm,alisema kuwa mwaka jana wote alikuwa ‘host’ kwenye mashindano ya kutafuta vipaji vya uigizaji (Tanzania Movie Talents) ambayo ilifanyika karibu mikoa yote,pia alikuwa bize na masomo katika chuo cha Magogoni akichukua kozi ya Public Administration.

‘’Mwaka jana wote sikufanya filamu kabisa kutokana na kuwa bize kwenye shindano la kutafuta vipaji vya uigizaji na pia shule nayo ilinibana kwahiyo sikuwa na muda wa kufanya filamu,’alisema Lulu.

Aidha alisema kuwa kwa sasa ameingia mzigoni kufanya filamu yake mpya ambayo hajaipa jina bado chini ya kampuni yake ya Proin Promotion ambayo itakuwa na wasanii mbalimbali kama Dude na wengineo.

‘Filamu hii inahusu maisha,mapenzi na komedi kidogo na kwa sasa hivi nitakuwa natoa filamu mbili kwa mwaka ndiyo utaratibu niliojiwekea,’aliongeza Lulu.

Cloudsfm.com

Lowassa Azidi Kuvunja Rekodi.......Msafara Wake Waingia Tabora Kwa Kishindo, Apata Wadhamini 9516

Waziri Mkuu wa Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akizungumza na WanaCCM waliofika kumdhani pamoja na wananchi wa Mji wa Tabora, kwenye viwanja vya ofisi za CCM Tabora Mjini, leo Juni 12, 2015. 
Waziri Mkuu wa Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akiwapungia mkono maelfu ya wana CCM waliofika kumdhamini pamoja na wananchi wengine, kwenye viwanja vya ofisi za CCM Tabora Mjini, leo Juni 12, 2015. 

Mh. Lowassa amepata udhamini wa wana CCM 9516 kwa mkoani Tabora, ikiwa ni muendelezo safari yake ya kutafuta wana CCM wa kumdhamini baada ya kuchukua fomu za kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi kimteue kuwania nafasi ya urais wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. 
Mh. Lowassa akisalimiana na Mmoja wa Wazee wa Mji wa Tabora. 
Waziri Mkuu wa Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akipokea majina kutoka kwa Naibu Katibu wa CCM Wilaya ya Tabora Mjini, Bi. Hidaya Rashid yenye idadi wanachama wa CCM 9516 waliomdhamini ili aweze kuteuliwa na Chama kuwania Urais wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. 
Waziri Mkuu wa Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akisalimiana Mzee Juma Nkumba, aliewahi kuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoani Tabora miaka ya nyuma.
Older Posts
© Copyright VIJIMAMBOZI Published.. Blogger Templates
Back To Top