"MAPEDESHEE NDIYO WANAWALIPA WASANII WA KIKE SIYO FILAMU"...LULU



ELIZABERTH Michael‘ Lulu’ amefunguka kuwa wasanii wa kike wa filamu wana biashara nyingine iliyojificha ndani ya ile ya filamu ambayo inawalipa zaidi.

Elizabeth Michael ‘Lulu’,akiwa kwenye pozi.

Lulu amepasua kuwa wasanii hao wanawategemea mapedejee kuendesha maisha yao huku wengi wakiamini kwamba mabinti hao wa Bongo Movie wanalipwa vizuri kutokana na filamu wanazoigiza.

“Ukweli hauko hivyo, hali hii inatokana na wengi wetu kudumaa na hatuwazi kufanya mambo makubwa kwa kuigiza na wasanii wakubwa lakini hakuna anayeliona hili,” alifafanua.

“Hakuna anayefirikiria kuigiza na wasanii wa kimataifa kama Ritha Dominic ili sanaa imlipe na wengi wanawategemee mapedejee au biashara zisizo rasmi, kwani filamu inaonekana ipo juu lakini wahusika wake wanalipwa kwa staili nyingine kabisa,” alisema

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright VIJIMAMBOZI Published.. Blogger Templates
Back To Top