Waziri wa JK ataka shule kufanya tambiko




Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mpwapwa mkoani Dodoma wakiwa katika moja ya mikutano ya Shule 


Mpwapwa. Ingawa Serikali ya Tanzania haiamini katika ushirikina wala matambiko, kuna watu mbalimbali na jamii tofauti zinaamini katika mambo hayo.

Serikali imekuwa ikipinga na kulaani vitendo vinavyoashiria ushirikina hata kuwashughulikia watu wanaonaswa wakishabikia imani hizo potofu.

Hata hivyo baadhi ya maeneo nchini bado watu wake wanaendeleza imani za kishirikina pamoja na matambiko.

Hata hivyo siyo jambo la kawaida kwa kiongozi hasa wa Serikali kusikika akihimiza kufanyika kwa matambiko ingawa kimsingi tukio hilo linahesabiwa kuwa ni namna ya kutafuta ufumbuzi kwa njia za kiakili na siyo ushirikina.
Ndivyo ilivyotokea hivi karibuni wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma.

Ni kama hadithi, lakini katika tukio la Februari 8 asubuhi, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alitoa maagizo ya kufanyika kwa tambiko muda mfupi baada ya kuwasili eneo la Sekondari ya Mpwapwa kwa ajili ya kutoa pole na kuwafariji wanafunzi wa kike ambao bweni lao liliteketea kwa moto.

Baada ya maelezo kutoka kwa mkuu wa shule hiyo pamoja na mbunge wa Jimbo la Mpwapwa Gregory Teu, naibu waziri aligeuka na kutoa maagizo ya kufanya matambiko mazito katika eneo hilo.

Ilivyokuwa

Mkuu wa Sekondari ya Mpwapwa, Nelson Milanzi alianza kwa kutoa simulizi ya tukio la moto ulioteketeza mabweni ambalo lilitokea Januari 20 mwaka huu akisema kuwa vituko vilianza siku moja kabla ya tukio.

“Wanafunzi walitoa maelezo kwamba kulikuwa na nyoka mkubwa aliyeonekana akishuka kutoka katika paa la bweni na alipodondoka chini, uliwaka moto mkubwa. Lakini cha ajabu, moto huo uliunguza shuka mbili za bluu mashati mawili na ghafla ulizimika. Majivu niliyakuta,” anasimulia Milanzi.

Mkuu huyo anasema kuwa tukio hilo lilikuwa na ajabu kiasi cha kumfanya akusanye wanafunzi wa kiume na walimu zaidi ya 10 na kuwapandisha katika dari na kuanza kufanya msako mkali, lakini hawakumuona nyoka huyo.

Siku iliyofuata, mambo yaligeuka, nyoka yule yule aliyeungua jana, alitua chini ghafla na safari hii kukiwa na mwanafunzi mmoja wa kike na moto uliwaka na kushika kasi ya ajabu, ambapo kila kilichokuwa ndani kiliteketea.
CHANZO:MWANANCHI

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright VIJIMAMBOZI Published.. Blogger Templates
Back To Top