Lowassa na Dk. Slaa ni marafiki wa Gwajima? Wanachokitaka UKAWA kabla ya Uchaguzi 2014… Zisikilize kutoka #PB


Jumatatu ya April 06 kati ya stori zilizosikika kwenye uchambuzi wa MAGAZETI kwenye #PowerBreakfast iko ya Askofu Gwajima kusema hawezi kuwatupa Lowassa na Dk. Slaa kwa kuwa ni marafiki zake wa siku nyingi, UKAWA kuidai Serikali mambo manne kabla ya uchaguzi, na madereva kugoma kurudi shule kwa kuwa hawana mikataba ya ajira wanazofanya.

Stori nyingine inahusu mtoto mlemavu kufungiwa darini miezi minne, Polisi kujiua kwa kujipiga risasi katika kituo cha Polisi Tabora, iko nyingine ya waasisi wa CCM kukubali utafiti ulioonesha Prof. Mark Mwandosya anafaa kugombea Urais 2015.

Rais Kikwete amesema Serikali ya awamu yake inajivunia mafanikio, Waziri Bernard Membe amewataka vijana wasikubali kutumika, kuna stori pia ya watu 1665 kukosa makazi kutokana na mvua kubwa iliyonyesha Simiyu.

Imeandikwa pia kuhusu bunduki nyingine kupotea katika mazingira ya kutatanisha kituo cha Polisi Tabora, watoto 21 wazaliwa katika mkesha wa Pasaka Iringa, wapenzi waliokamatwa kwa kuuza tiketi za kwenda peponi Uingereza na waumini Shinyanga wakaguliwa kabla ya kuingia kwenye ibada ya mkesha wa Pasaka.
Hizi zilisikika kwenye show hiyo..
88.1 Clouds FM inasikika ukiwa Mwanza.
Kama ulipitwa bonyeza play hapa chini kusikiliza uchambuzi wa story zote za Magazeti ya leo…
 SIKILIZA HAPA

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright VIJIMAMBOZI Published.. Blogger Templates
Back To Top