WANUSA KIFO,BODABOYA YAO YACHOMWA MOTO BAADA YA KUPORA MKOBA,SIMU

Vijana wawili wa bodaboda walikoswakoswa kuuawa baada ya kupora mkoba uliokuwa na simu wa mwanamke aliyekuwa akipita njia. Tukio hilo lilitokea Jumanne iliyopita, saa 1.30 usiku maeneo ya Sinza Afrika Sana, pembeni ya Baa ya Hongera ambapo inadaiwa ni eneo hatari kwa wizi huo.


Mmoja ya watuhumiwa akiwa hoi baada ya kupata kipigo



Shuhuda wa tukio hilo amesema kuwa tabia ya baadhi ya vijana kutumia usafiri wa bodaboda kupora watu simu na mikoba, hasa wanawake, imekua kawaida; na kwamba siku hiyo arobaini ya vijana hao ilikuwa imefika.

“Sisi tulikuwa pale baa tunakunywa, mara tukamsikia mtu akipiga kelele za mwizi…mwiziii, ile kutoka ndiyo tukawaona hawa vijana wawili wakihangaika kuwasha bodaboda yao ili wakimbie.


Askari polisi aliyeokoa maisha ya mtuhumiwa akiwa katika eneo la tukio



“Yaani ilikuwa ni Mungu tu maana bodaboda isingegoma kuwaka, tusingewapata. Basi raia wenye hasira kali wakaanza kuwashushia kipigo, aliyekuwa akiendesha pamoja na yule dada aliyeibiwa wakachukuliwa hadi Kituo cha Polisi Mabatini huku aliyekwapua akipewa kipigo,” alisema shuhuda huyo.

Hata hivyo, kijana huyo aliponea chupuchupu kuchomwa moto, kwani waliokuwa wamefuata mafuta ya petroli waliporudi walimkuta trafiki akizuia asiuawe.Kufuatia zuio hilo, raia hao walihamishia hasira zao kwenye kuichoma moto bodaboda kisha mtuhumiwa akachukuliwa hadi polisi kwa hatua zaidi za kisheria


Bodaboda iliyokuwa inatumiwa na vibaka hao ikiteketea kwa moto baada ya kuchomwa na washeria mkononi

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright VIJIMAMBOZI Published.. Blogger Templates
Back To Top